Wednesday 24 July 2013

TAIFA STARS YATUA KAMPALA KWA MBWEMBWE, KIM ATAMBA KUIFUNGA THE CRANES

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imewasili nchini Uganda jioni ya leo katika uwanja wa ndege wa Entebe Kampala tayari kuikabili Uganda the Cranes kwa mechi ya marudiano kutafuta tiketi ya kucheza katika mashindano ya CHAN.

Kikosi hicho chenye wachezaji 20, kiliwasili muda mfupi baada ya saa kumi alasiri huku wachezaji na benchi la ufundi wakiwa na matumaini makubwa.

Akiongea mara baada ya kuwasili Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen alisema wamejiandaa vizuri wakiwa Mwanza na ana imani kikosi chake kitabadili matokeo ya awali ambapo Stars ilifungwa 1-0 na Cranes Jijini Dar es Salaam.

Alisema licha ya kuwakosa wachezaji Shomari kapombe na Mwinyi Kazimoto, ana imani na kikosi chake kuwa kitafanya makubwa Jijini Kampala.

“Tumekuja kubadilisha mahesabu kwani tumejiandaa vizuri kabisa,” alisema Poulsen.



Mechi hii ni gumzo kubwa Jijini Kampala kwani baadhi ya waganda wana hofu kuwa henda wakafungwa nyumbani kwao.

Mechi hii itapigwa katika Uwanja wa Namboole Jijini Kampala Jumamosi hii saa kumi jioni.

Mashindano ya CHAN yanatarajiwa kufanyika Januari mwakani nchini Afrika Kusini.

Wachezaji na Benchi la Ufundi (Taifa Stars) wakiwasili Uwanja wa Ndege wa Entebe nchini Uganda jioni ya leo tayari kuikabili Uganda The Cranes Jumamosi hii.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako