Wednesday 21 January 2015

LIVERPOOL YACHOMOA KIPIGO KUTOKA KWA CHELSEA

BAO la Raheem Sterling dakika ya 59 limeipa Liverpool sare ya 1-1 nyumbani na Liverpool katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Kombe la Ligi England, maarufu kama Capital One Cup.

Katika mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Anfield, Eden Hazard alitangulia kuifungia Chelsea kwa penalty dakika ya 18, baada ya yeye mwenyewe kuchezewa rafu na Emre Can

MICHUANO MECHI ZA AFRCON

MIAMBA ya soka kutoka Magharibi mwa Afrika, Ivory Coast imeanza kwa sare ya 1-1 dhidi ya Guinea katika mechi ya kundi D , michuano ya mataifa ya Afrika inayoendelea huko Guinea ya Ikweta.
Guinea walikuwa wa kwanza kufunga goli katika dakika 36’ kipindi cha kwanza kupitia kwa nyota wake Mohamed Yattara, hata hivyo Ivory Coasta walisawazisha dakika ya 72’ kupitia kwa Seydou  Doumbia.
Nayo mechi ya pili ya kundi kund hilo baina ya Mali na Cameroon imemalizika kwa sare ya 1-1.
Mali waliandika bao la kuongoza dakika ya 71’ kupitia kwa Yambou Yatabare, lakini Simba wasiofugika, Cameroon wakasawazisha kupitia kwa Ambroise Oyongo Bitolo.
Kufuatia kumalizika kwa mechi za kwanza za kundi D, michuano hiyo leo inaendelea kwa mzunguko wa pili wa makundi.
Timu za kundi A zinaanza kutupa karata yao ya pili ambapo mechi ya kwanza itawakutanisha wenyeji Guinea ya Ikweta dhidi ya Burkinafaso ambao walipoteza mechi ya kwanza kwa mabao 2-0 dhidi ya Gabon.
Mechi ya pili inayoanza majira ya saa 4:00 usiku leo, itawakutanisha Congo na Gabon.


Tuesday 13 January 2015

CHRISTIANO RONALDO MCHEZAJI BORA WA DUNIA FIFA BALLON D' OR KWA MARA YA 3 SASA

C 7


Christiano Ronaldo ndiye mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora Ulaya na Duniani kote maarufu kama Ballon d'Or.
Ronaldo mwenye miaka 29, ametwaa tuzo hiyo kwa kumbwaga mpinzani wake mkubwa Lionel Messi wa Barcelona na kipa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Raia huyo wa Ureno ametwaa tuzo hiyo kwa mara ya pili mfululizo hii ikiwa ni mara yake ya tatu kutwaa tunzo hiyo kwa kuwa mara ya kwanza aliibeba 2008 akiwa na Manchester United.

Mwaka jana, Ronaldo akiwa na Real Madrid aliiwezesha kutwaa ubingwa wa Ulaya, Copa del Rey, Uefa Super Cup, pia ubingwa wa dunia huku yeye akifunga mabao 56 katika mechi 51.

Dakika chache baada ya kutwaa tuzo ya mchazaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amefunguka wazi kwamba anataka kumfikia mpinzani wake Lionel Messi.


Ronaldo ameeleza kufurahishwa kwake na kutwaa tuzo yake ya tatu lakini akasisitiza angefurahi kuichukua kwa mara ya nne kama ilivyo kwa lionel Messi.

Tuesday 6 January 2015

HALI YA MCHEZAJI CHRISTOPHER ALEX MASSAWE

Wachezaji wa Simba ambao walishiriki katika kikosi kilichoing’oa Zamalek mwaka 2003 wameamua kumchangia mwenzao Christopher Alex Massawe.
Kikosi cha Simba 2003
 
Massawe yu mgonjwa taabani huko kwao Dodoma. Hali ambayo imewafanya Simba walioifunga Zamalek, Massawe akifunga penalti ya mwisho iliyoihakikishia Simba ushindi.

Kiungo huyo anaumwa na imeelezwa anasumbuliwa na kifua kikuu ingawa bado jambo hilo halijatolewa ufafanuzi na familia yake.

Akizungumza, Boniface Pawasa ambaye alicheza namba tano katika mechi hiyo amesema wanaandaa mechi ya kirafiki ikiwa Lengo ni kupata mechi ambayo itamsaidia ndugu yetu kupata matibabu.

“Wikiendi hii tunaweza kucheza pale Karume kama hakutakuwa na mechi ya daraja la kwanza. Hili ni jukumu letu, wadau wajitokeze.
 
“Tayari baadhi ya waliocheza siku hiyo wamejitokeza, Emmanuel Gabriel na Victor Costa tumeishakubaliana," alisema Boniface Pawasa

Monday 5 January 2015

PANYA ROAD NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM



Vijana 36 wanaodaiwa kuwa ni wa kikundi cha uhalifu kinachojulikana kama PANYA ROAD wanashikiliwa na jeshi la polisi nchini kwa tuhuma za kufanya vitendo vya uhalifu na kuleta hali ya taharuki katika maeneo mbalimbali ya Jiji la DSM hapo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini DSM, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini ADVERA BULIMBA amesema kwa sasa hali imedhibitiwa na kuwataka Wakazi wa jiji la DSM kuendelea na shughuli zao bila wasiwasi.
Vijana hao wamekuwa na tabia za uporaji wa mali za raia kwa kutumia silaha za mapanga na visu wamekuwa tishio kwa kipindi kirefu jijini Dar es salaam hivyo taarifa za kushikiliwa kwao zimekuwa za faraja kwa watanzania na wakazi wa Dar es salaam kwa ujumla

BONDIA KIMWERI ALIYEKO NCHINI AUSTRALIA KUTUA JIJINI DAR ES SALAAM



Mwezi Februari mwaka huu Super D atakuwa na ugeni mkubwa wa bondia Mtanzania anayefanya kazi zake nchini Deer Park, Victoria, Australia, Omari Kimweri ambaye anatua nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanamasumbwi wa Tanzania.
Akizungumza jijini Dar es salaam hapo jana, Super D alisema kuwa ujio wa Kimweri ni fursa nyingine adimu kwa mabondia wa Tanzania katika kuona ni vipi wanaweza kutimiza ndoto zao za kutoka kimaisha kupitia mchezo huo.

Amesema kuwa Kimweri atatua akiwa na vifaa mbalimbali vya masumbwi ambapo pia atatoa mafunzo na mbinu mpya zinazotumiwa na mabondia wa nje pamoja na kushuhudia mapambano kadhaa yatakayofanyika kwa kipindi atakachokuwapo hapa nchini.

“Kimweri anakuja akiwa na msafara wa watu kadhaa, akiwamo mwanasoka wa kike, Melanie Gines ambaye ni raia wa Hispania. Akiwa hapa nchini, Melanie atapata fursa ya kukutana na wanasoka wa kike wa hapa , kwani amechezea timu nyingi za Ulaya,  huko Hispania,”
Amesema kuwa ujio wa Kimweri umewezeshwa kwa kiasi kikubwa na promota wake, Brian Amatruda ambaye ni miongoni mwa mapromota maarufu nchini kwao Australia, akiwa amekubari kutoa baadhi ya vifaa vya kisasa kutoka Hispania na Marekani kwa ajili ya ziara hiyo.

Super D anasema kuwa Kimweri ambaye ni bingwa wa WBO, atatua nchini akiwa na mikanda yake yote aliyowahi kutwaa, ukiwamo wa ubingwa wa Australia, lengo likiwa ni kuwahamasisha vijana wa kitanzania kujikita zaidi katika ndondi.