Monday 15 July 2013

MAU WA MAHOKAz AZUNGUMZIA KOMEDI ZA BONGO

MCHEKESHAJI mahiri katika tasnia ya filamu Swahiliwood Maulid Ali ‘Maufundi’ amesema kuwa katika historia ya maisha yake hawezi kuigiza katika komedi, Mau anasema kuwa hadhi ya Komedi imepotea baada ya kuibuka Komedi za kukurupuka na kujikusanya na kurekodi bila ya kutumia muswada (Script) ambalo linaua sanaa hiyo.
Maufundi akiwa location kurekodi filamu ya Chips kuku.
“Ninajua thamani yangu siwezi kuigiza katika Komedi changanyikeni, hawa ndio wanaotuharibia kwa kukurupuka na kurekodi vuluvulu, ndio maana komedi zetu zinaanzia gengeni kuvaa nguo mbovu mbovu na kuwa wachafu, kila siku nawaambia wachekeshaji wenzangu kuchekesha siyo lazima kuwa wachafu tunatakiwa kubadilika kuwa smart,”anasema Mau.
Msanii huyo ambaye kwa mwaka huu amekuwa gumzo katika tamasha la filamu la kimataifa la ZIFF kwa kuonyesha filamu yake ya Chips kuku iliyotikisa Ngome Kongwe, alisema kuwa mbona wasanii kama Martin Lawrence, Fresh Prince Queen Latifa na wengineo wanachekesha huku wakiwa nadhifu, naye anakuwa kama hao.
Lakini jambo lingine ambalo linamfanya ashindwe kuunga na wachekeshaji wengine ni maslahi, kutokana na watayarishaji wengi wa komedi kudharauliwa na kulipwa fedha kidogo wakati wao ni kipenzi cha watazamaji wengi, Mau kawahimiza wachekeshaji kubadilika na kuwa na misimamo kwa ajili ya fani yao, pia Mau anasema wasanii wengi kufungia kama Ng’ombe na kuigiza kwa pamoja inaua sanaa hiyo, kwanii kila mtu anataka kumfunika mwezake.

SOURCE: Filam Central Tanzania

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako