Tuesday 23 July 2013

SCORPION GIRLS WAVURUGANA



MEMBA wa Kundi la Scorpion Girls, Isabela Mpanda ‘Bela’ na Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ wametofautiana hadi kufikia hatua ya kutukanana na kutupiana nguo nje.
 

Mpango mzima ulitokea hivi karibuni Kijitonyama jijini Dar, nyumbani kwa Isabela ambapo chanzo cha ugomvi huo ni baada ya Isabela kumsifia mtandaoni X-memba wa kundi lao, Jacqueline Pentezel ‘Jack wa Chuz’ kwa kununua gari, ndipo Kabula  alipokasirika na kuanza kumtukana Bela na mama yake matusi ya nguoni.
“Sikumuelewa kabisa Jini, kumsifia Jack kuhusu kumiliki gari ndiyo kumemfanya anitukane? Iliniuma sana na sitamsamehe, bora kila mtu achukue hamsini zake, nguo zake nilimtupia nje,” alisema Bela na kusisitiza kufanya muziki peke yake kwa sasa.


No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako