Monday 22 July 2013

UBELGIJI YAPATA MFALME MPYA


Nchi ya Ubelgiji jana Jumapili imepata Mfalme Mpya wa 7 baada ya mzee wake Mfalme Albert kutawala kwa kipindi cha miaka 20.

Mfalme Prince mwenye umri wa miaka 53 ameapishwa jana kuwa mfalme mpya wa nchi ya ubeligiji Mfalme Philippe sasa anachukua kiti hicho cha kifalme kutoka kwa baba yake mfalme Albert II (79) ambaye amejiuzulu kutokana na sababu za kiafya.
Mtawala mpya wa Ubelgiji King Philippe mwenye umri wa miaka 53 ameapishwa bungeni Julai, 21 2013 kwa kufuata katiba ya nchi hiyo
“naapa kwa heshima ya katiba na sheria za watu wa ubelgiji, kuwa nitalinda uhuru wa nchi hii na kulinda mipaka yake” Mfalme Philippe ameyasema hayo kwenye kiapo chake
Ameongeza kuwa baba yake ametawala kwa muda wa miaka 20, ameweza kutawala kwa kujiamini na kutekeleza yote kwa upendo na umoja na kwa upande mwingine alikuwa makini na kutekeleza majukumu kiuaminifu.
Wakishangilia siku ya uhuru wan chi yao, wabelgijia wamejumuika kwa pamoja kwenye sherehe za kuapishwa kwa mfalme wao mpya.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako