Saturday 31 August 2013

PENNY ASEMA YEYE NA DIAMOND NDO KALI YAKE



Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Penny ambaye sasa anapika na kupakuwa kwa Diamond alisema anamuamini sana mpenzi wake huyo na kwamba kuhusishwa kwake na mambo ya mademu kila kukicha kunatokana na kazi yake.


Mara baada ya hivi karibuni kuandikwa habari iliyoeleza kwamba nchini Kenya kuna demu aliyemzimikia ile mbaya mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ huku akiahidi kumpa penzi zito, mpenzi wa msanii huyo Peniel Mwingilwa ‘Penny’ ameibuka na kudai hatishwi na maneno hayo.


“Yatasemwa mengi lakini siwezi kumuacha Diamond, namuamini na najua haya yote yanayotokea ni kwa sababu ya kazi yake kwa hiyo wanaodhani mimi nitayachukua na kuamua kumuacha watasubiri sana, ndiyo kwanza penzi letu linazidi kushamiri,” alisema Penny.

Friday 30 August 2013

NAY WA MITEGO NA MADAM RITA HAWANA TATIZO


PATA VIDEOs ZA KWENYE UZINDUZI WA VIDEO MPYA YA DIAMOND

 
Waalikwa wakipiga Story na Shemeji yao (Mke mtarajiwa wa Diamond - Penny) ndani ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Diamond akimfungulia na kumuwashia gari aliyomzawadia Mzee Ngurumo nje ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Diamond akiwakaribisha wageni waalikwa ndani ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Diamond akiomba idhini ya kwenda kumpa gari yake Mzee Ngurumo Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Diamond na wacheza shoo wake wakiburudisha hadhira kwa track hiyo mpya ndani ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video hiyo
 
Picha ya Diamond akiwa na wadau wa muziki ndani ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Hii ndiyo gari aliyopewa Mzee Ngurumo wakati wa Uzinduzi wa Video ya Diamond katika Hotel ya Serena
 
Baadhi ya wadau waliokuwepo ndani ya ukumbi wa Serena Jana usiku katika uzinduzi wa Video ya my number one
 
Behind the scene ya Video ya my number one ikielezewa na Mhusika Mkuu Diamond Plantinium
Hii ndiyo Video yenyewe ya my number one ikioneshwa kwenye moja ya Screen zilizokuwepo ndani ya Ukumbi wa Serena

WATOTO WATENGANISHWA NA MADAKTARI TANZANIA

Jopo la Madaktari Bingwa Saba wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Mifupa ya hospitali hiyo (Moi), wamefanikiwa kuwatenganisha pacha waliokuwa wameungana kiwiliwili.Iliwalazimu mabingwa hao kutumia saa nne kufanikisha upasuaji huo. Mmoja wa watoto hao waliotenganishwa, amelazwa kwenye Wodi ya Uangalizi Maalumu (ICU) Taasisi ya Mifupa Moi wakati kiwiliwili kingine kilifariki.(P.T)
 
Jopo la madaktari waliofanikisha upasuaji huo ni; bingwa mstaafu wa watoto ambaye aliitwa maalumu kwa kazi hiyo, Petronila Ngiloi, Dk Robert Mhina (mifupa) na Profesa Karim Manji aliyekuwa akifuatilia kwa karibu mapigo ya moyo. 
Wengine ni Dk Karima Khalid aliyekuwa akiratibu dawa ya usingizi, Dk Hamis Shaaban (ubongo na uti wa mgongo), Dk Zaitun Bokhary (bingwa upasuaji watoto) na Dk Nyangasa (moyo na mishipa ya fahamu) 
Akizungumza baada ya upasuaji huo, Dk Shaaban alisema walimfanyia vipimo mtoto ambaye hakuwa amekamilika na kugundulika kuwa hakuwa amekamilika viungo vyote achilia mbali kutokuwa na kichwa na macho pia hakuwa na moyo, figo, tumbo, maini ila alikuwa na uti wa mgongo.
"Uti wa mgongo ulikuwepo na ndio uliokuwa umeshikana na mwenzake na kuna mshipa mmoja wa fahamu ulikuwa unafanya kazi ndio maana alikuwa ukimgusa anachezesha mguu."
Alisema kinachoratibiwa kwa sasa ni kuangalia dawa ya usingizi aliyopewa mtoto ambaye anaendelea kupumua na kwamba ndani ya saa 24, dawa ya usingizi waliyomuwekea mtoto huyo itakuwa imeisha na ataanza kunyonya kama kawaida.
Upasuaji
Kazi ya upasuaji huo ilianza saa mbili asubuhi kwa mtoto huyo wa jinsi ya kike aliyetimia kuchukuliwa vipimo mbalimbali ikiwemo CT Scan, MRI, Ultra sound na vingine vingi kabla ya upasuaji kamili kuanza saa tano asubuhi.
Dk Shaaban alisema ni mara ya kwanza kwa Moi kufanya upasuaji wa aina ile na kwamba mara nyingi wamekuwa wakifanya upasuaji wa watoto wanaozaliwa na vichwa vikubwa pamoja na mgongo wazi ambao tatizo hilo linasababishwa na upungufu wa madini ya folic acid.
Kabla ya upasuaji kuanza, mama wa mtoto huyo Pili Hija (24) alitumia muda wa nusu saa kufanya maombi maalumu ya kumwombea mtoto wake kisha kuwaruhusu madaktari kuendelea na upasuaji huo.
Akizungumza muda mfupi baada ya kuruhusiwa kumwona mtoto wake, Hija alisema: "Ninamshukuru Mungu kwa yote na nazidi kumwomba amjalie mwanangu apone kabisa, nawashukuru na nitazidi kuwaombea madaktari wanaomtibu mwanangu."Alijifungulia nyumbani Agosti 18 maeneo ya Jang'ombe, Zanzibar watoto pacha walioungana mmoja akiwa amekamilika viungo vyote na mwingine akiwa na kiwiliwili.

NAFASI ZA MASOMO CHUO KIKUU CHA WAISLAAM MOROGORO


Thursday 29 August 2013

ASKOFU MOSES KULOLA AFARIKI DUNIA


Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde zinasema kuwa Askofu Mkuu wa Evangelistic Assemblies God Tanzania, Moses Kulola amefariki dunia takriban dakika 25 zilizopita.
Kwa mujibu wa taarifa za kuaminika  kutoka kwa watu wa ndani wa familia hiyo, zinaeleza kuwa Askofu Kulola amefariki katika hospitali ya AMI (African Medical Investments) iliyopo Slipway jijini Dar es Salaam.
Askofu Kulola, ambaye amezaliwa mwaka 1928, amekuwa akisumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu na hata kufikia hatua ya kupelekwa nchini India kwa matibabu.
Katika uhai wake, amepata watoto wengi wa kiroho ikiwemo Dr Daniel Kulola, Mchungaji Florian Katunzi, Zakaria Kakobe, Mzee wa Upako, Maboya, Mwasota na wengineo wengi.
BWANA ametoa na BWANA ametwaa, jina la BWANA lihimidiwe. 

HISTORIA YA ASKOFU MOSES KULOLA
Moses Kulola, alizaliwa mwezi Juni 1928, katika familia ya watoto kumi, na watano kati yao bado ni hai. alisajiliwa katika shule ya kwanza mwaka 1939 iitwayo Ligsha Sukuma shule ya misheni baada ya Ligsha, alijiunga na taasisi ya usanifu mwaka 1949. Alibatizwa mwaka 1950 katika Kanisa la AIC Makongoro.
Ni mume wa Elizabeth na wamezaa watoto10 ambapo saba bado hai.alianza kazi za kimisionari mwaka1950 japokuwa aliitwa mwaka 1949 mara tu baada ya kubatizwa.
Mwaka 1959 alianza kufanya kazi serikalini, wakati huo huo akihubiri Injili katika miji na vijiji. Utumishi wake mkubwa kwa nchi ulifika mwisho mwaka 1962, ambapo aliamua kujitolea moja kwa moja nguvu zake zote, mwili na nafsi. Mwaka 1964 alijiunga na chuo cha kiteolojia na 1966 alitunukiwa stashahada.
Hakuacha elimu pale tu, aliendelea na masomo mbalimbali ambapo alitunukiwa vyeti mbalimbali katika mataifa mbalimbali.
Alihudumu kikazi kwa miaka miwili kama Mchungaji kabla ya kuwa mpentekoste mnamo 1961-1962, alifanya kazi katika kanisa la TAG 1966 mpaka 1991 ambapo aliamua kuanzishaa makanisa Evangelistic Assemblies God (EAGT), ambapo yalifanikiwa kukua kwa kasi kubwa katika nchi za Tanzania, Zambia , Malawi na kwa ujumla kuna makanisa yapatayo 4000 katika nchi mbalimbali yakiwemo makubwa na madogo Askofu Moses Kulola anayeongoza makanisa elfu nne, Askofu Msaidizi wake ni Mwaisabila.
Askofu Kulola aliyeketi akiwa na waimbaji wa injili nchini Mwinjilisti Faustin Munishi mkono wa kushoto pamoja na Emmanuel Mwasota, mwanzoni mwa mwaka 1970

Mchakato wa kuongoza makanisa elfu nne si rahisi na kwamba kumefanyika mgawanyiko wa majimbo yasiyopungua 34 ya kazi na kanda tano kwa ajili ya kurahisisha kazi na kila kanda na jimbo lina mwangalizi wake.  
Nampenda sana Askofu Moses Kulola maana anafanya kazi ya MUNGU kwa moyo na kwa mujibu wa kitabu cha historia yake Askofu Kulola amezunguka Tanzania nzima tena wakati mwingine kwa kutembea kwa miguu na kwenye mazingira magumu sana kiasi kwamba ni wito mkuu wa MUNGU mkuu alionao Askofu Kulola na kwa miaka zaidi ya 60 amekuwa akihubiri neno la MUNGU na hadi sasa MUNGU anamtumia sana, katika mkutano uliopita wa askofu Kulola pale viwanja vya jangwani jijini Dar es salaam maelfu ya watu walihudhulia na wengi sana kufunguliwa na injili anayohubiri askofu Kulola ni injili iliyonyooka na akiwataka wanadamu kumpa YESU KRISTO maisha yao ili wapate uzima wa milele bure.
Ukiacha mengi ambayo Mungu anaendelea kumtumia mtumishi wake huyu, kuna suala la nywele zake, askofu Kulola kama tulivyowahi kuandika siku zilizopita, hajanyoa nywele zake kwa takribani miaka 47 sasa, kwakuwa hakupendezwa na suala la kwenda salon kunyoa nywele zake hivyo akamwambia Mungu nywele alizokuwa nazo kwa wakati huo zisikue zaidi au kupungua, na ndivyo ilivyo mpaka sasa wembe haujapita kichwani mwake.

BAADA YA KUPIGIWA KELELE KANGA MOJA NDEMBENDEMBE BALAA JINGINE LAJA



Uchunguzi Wa kina takriban miezi kadhaa umebaini kuwepo kwa stili nyingine ya uchezaji ndembendembe, kwamba staili hiyo mpya ya uchezaji wa muziki wa mwambao kwa kulowanisha tisheti laini nyeupe kwa maji na kusababisha chuchu kuonekana sawia, inazidi kushika kasi kama moto wa kifuu Jijini Dar es Salaam.
Imebainika kuwa staili hiyo ambayo ilianzia Pwani ya Kenya, sasa inatumiwa kudhalilisha warembo Uswahilini hasa kwenye ngoma maarufu za ‘kigodoro’ ambazo huchezwa bila kujali rika mbalimbali zinazokuwa zimechanganyikana.
Habari zinaeleza kuwa katika uchezaji huo, sharti ‘nido’ ya mrembo iwe saa sita ili kuwavutia na kuwaridhisha wanaume kimahaba ambao kazi yao huwa ni kuwatuza fedha baada ya kufurahishwa kwa kutazama uchezaji huo na wengine kuondoka nao kwenda kuvunja amri ya sita.
Ilifahamika kuwa staili hiyo imewavutia wengi na vikundi vya uchezaji huo vimeanza kuundwa japo havijapata umaarufu mkubwa.
Mamlaka na wizara husika zinatakiwa kukemea kwa nguvu zote kwani huo ni mwanzo mwingine wa mmomonyoko wa maadili ya Kitanzania na ongezeko la maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi (VVU)

AC MILAN YAFUZU KWA HATU ZA MAKUNDI


AC Milan ya Italia kwa mara ya kumi na moja katika muda wa miaka kumi na mbili iliyopita imefuzu kushiriki Kombe la Klabu Bingwa baranai Ulaya.
Milan imeilaza PSV Eindhoven kutoka Uholanzi kwa mabao 3-0.
Baada ya kutoka sare ya 1-1 na Uholanzi katika mechi ya awamu ya kwanza, Kevin Prince alifunga mabao mawili yaliyoiweka timu yake mbele, naye Mario Balotelli akaongezea la tatu na hivyo kuihakikishia mabingwa wa zamani wa kombe hilo nafasi katika raundi ijayo kwa jumla ya mgoli 4-1.
Katika matokeo mengine iliyochezwa siku ya jumatano, Zenit St Petersburg iliikwaruza Pacos Ferreira kwa mabao manne kwa mawili na kufuzu kwa hatua ijayo kwa jumla magoli manane kwa matatu.
Kwingineko, mabingwa wa Jamhuri ya Czech, Viktoria Plzen walishinda wenyeji wao Slovenia Maribor kwa bao moja kwa bila na kujikatia tikiti ya raundi ijayo ya makundi ya kinyang'anyiro cha kuwania Kombe la Klabu Bingwa Barani Ulaya.
Viktoria Plzen imesonga mbele na jumla la magoli 4-1.
Klabu hizo zitajiunga na Arsenal Schalke, Steaua Bucharest na Austria Vienna ambazo zote zilishinda mechi zao siku ya Jumanne katika hatua ya makundi.

COCA COLA WATEMBELEA DTV (NI WAKATI WAO)

Wawakilishi kutola Kampuni ya Coca cola wakipata maelezo kutoka kwa Mrusha Matangazo (Chriss Milinga-hayupo pichani) ndani ya Chumba cha kurushia matangazo ya DTV
Wawakilishi kutoka Kampuni ya Coca cola wakipata maelezo kutoka kwa Mrusha Matangazo (Chriss Milinga) ndani ya Chumba cha kurekodia vipindi vya DTV
Wawakilishi kutoka Kampuni ya Coca cola wakiwa Studio za DTV
Wawakilishi kutoka Kampuni ya Coca cola wakiwa Studio za DTV
Wawakilishi kutoka Kampuni ya Coca cola wakitoka Studio za DTV kuelekea eneo la kurushia matangazo
Wawakilishi kutoka Kampuni ya Coca cola wakipata maelezo zaidi kutoka kwa studio manager (Hayupo Pichani)

ZAIDI YA WATU 40 WAFARIKI KWENYE AJALI KENYA


Takriban watu 41 wanadaiwa kufariki baada ya basi moja la abiria lililokuwa likitoka Nairobi kuelekea Homabay Magharibi mwa Kenya kuanguka na kubingirikia mara kadhaa katika eneo la Narok.
Polisi wamethibitisha kuwa miongoni mwa waliofariki ni watoto wanne.
Mkuu wa polisi wilayani Narok Patterson Maelo amesema kuwa dereva wa basi hilo alishindwa kulithibiti katika eneo la kona na hivyo basi hilo kupoteza mwelekeo na kuanguka.
Maafisa wa shirika la msalaba mwekundi ambao tayari wamefika katika eneo la tukio hilo wamesema kuwa watu wengine 33 waliojeruhiwa wamesafirishwa hadi hospitali ya wilaya ya Narok kwa matibabu.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ni miongoni wa viongozi waliotuma salamu zao za rambi rambi kwa jamaa na marafiki wa abiria waliouawa.
Katika ripoti iliyochapishwa katika mtandao wake wa twitter, rais Kenyatta ametoa amri kwa idara ya polisi kuchukua hatua dhidi ya wamiliki wa magari ya umma wanaokiuka sheria za barabarani.
SOURCE: BBC