Wednesday 17 July 2013

KIFAA KIPYA KUTOKA KAMPUNI YA GOOGLE


Mwanzoni mwa mwaka huu, Google iliniuliza kama nitapenda kujaribu kutengeneza programu ambayo itakua inahusiana na matumizi mbalimbali ya google glass, kwakuwa hua napenda kujaribu kufanya kazi mbalimbali nilisoma maelezo niliyopewa na Google na nilivutiwa sana.
Matumizi ya programu na tecknolojia ya Google glass imekua ni ndoto ya muda mrefu ya watumiaji wa tecknolojia mpya ambao wamekua wakiutazama ulimwengu kama sehemu ambayo mawasiliano yanakua karibu nao sana.
Google Glass inaweza kutupa ukweli wa ndoto ya mda mrefu ambayo wengi wamekuwa wakiihitaji, lakini kwa kutekeleza hilo kunaibuka maswali mengine mapya, je bado tutakua tunahitaji zaidi ya hapo wakati tayari tunaitumia google glass? Je itafanya maisha kua magumu au itayarahisisha? Na je maelekezo yake ya usiri (privacy) ya mtu yatakua yanajali utamaduni?  
Mdahalo ndo kwanza umeanza, kwa upande wangu nafikiri tatizo kubwa la mifano mingi ya tecknolojia kama google glass ni kwamba msisitizo unawekwa sana kwenye tecknolojia yenyewe kuliko kwenye namna halisi ya uvaaji au utumiaji wake. Ili kuongeza maombi ya idadi ya watumiaji wakati Google glass ikiingia rasmi sokoni, Google itazingatia kwa makini njia ya kuunda mfumo mzuri ili kuepuka kuonekana kama kikwazo.
Itakua vizuri kuweka mahusiano mazuri na wabunifu mbalimbali wa miwani (glass) kama Tom Ford au Ray-Ban ili kutengeneza kitu ambacho kitaridhisha watu na watamani kuvaa. Nilikosa amani nilivyokua natakiwa kutoa maelekezo kwa ishara , hili pia ni tatizo langu na Siri pamoja na tecknolojia nyingine zinazotumia sauti kutoa maelekezo (voice-activated technology), nani anataka kuwa mjinga kuongea peke yake na kompyuta. Kwa saivi nilipendekeza kwa wawakilishi wa Google kwamba labda wanaweza kuwa na mawani yanayoweza kutambua aina Fulani ya lugha ya ishara na badae mtu anaweza akavaa pete au bangili yenye kifaa kidogo ambacho kina uwezo wa kusoma matendo yako na kuyawasilisha kwa mawani.
 Miezi michache ijayo baada ya kuingia sokoni Google Glass itakua na ushindani wa ghafla na tecknolojia nyingine zenye matumizi ya tecknolojia ya mawani kutoka kwa Apple na Samsung. Apple inatumia inchi 1.5 OLED screens ambazo zinafaa kwa “iwatch” , Samsung imethibitisha maendeleo ya smartwatch, na inasemekana kwamba mbinu ya smartwatch itakua rahisi na inayokubalika zaidi kutumia japokua haina huduma kubwa ya mawasiliano kama tecknolojia nyingine.
Karne ya tecknolojia ya kuvaa mawani ambayo google glass na smartwatches inatupeleka itakua kama soko la technolojia ya smartphone miaka saba iliyopita. Utaratibu mmoja naouona unatawala tecknolojia hii mpya ni kwamba ili tecknolojia ya mawani ilete maana inatakiwa kuyaboresha maisha yetu ipasavyo na sio kuyafanya yawe magumu au kuyaingilia bila mpangilio. 

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako