Wednesday 17 July 2013

MJI MZURI NA ULIOPANGIKA DUNIANI

Kisiwa cha Palm ni kisiwa kilichopo Dubai, United Arab Emirates (UAE), pembezoni kwa Persian Gulf, kimebuniwa na Nakheel properties kwa matumizi ya kibiashara pamoja na kuishi kasha kikaendelezwa kwa hisani ya UAE.
Muundo wake kama unavyoonekana ni kama mti na kisiwa kina ukubwa wa Kilometer za mraba 520, ambapo kuna hotel zaidi ya 100 za kufahari zenye fukwe nzuri, migahawa, maduka, maeneo ya michezo pamoja na eneo la mazoezi.
Kisiwa hicho kimejengwa mwaka 2002 na kumalizika October 2006.
Kisiwa cha palm kilitangazwa kwa maendeleo octoba 2004. Makadirio ya mwanzo ya muundo na ukubwa wake yalikuwa mara nane ya ukubwa wa palm Jumeirah na mara tano ya ukubwa wa palm jebel Ali. Kisiwa cha Palm Deira kinalengwa kuwapa makazi watu milioni moja. 
Mwanzo muundo wa eneo la kisiwa ulionekana kuwa na ukubwa wa kilometa14 kwa kilometa 8.5. kutokana na mabadiliko ya kina cha gofu ya Persia kisiwa cha palm Deira kilibadilishwa muundo wake mwezi wa tano mwaka 2007. Mabadiliko hayo yalikua na muundo mpya wa kilometa 12.5 kwa 7.5
Mapema octoba 2007, asilimia 20 ya ardhi ya kisiwa cha Palm (millioni 200 cubic meta za ardhi) ilikua tayari imemalizika kuandaliwa kwa shughuli mbalimbali za maendeleo na eneo hilo lilikua linatumika rasmi. 
Mwanzoni mwa mwezi wa nne 2008 Nakheel (kisiwa cha palm) kilitangaza kwamba zaidi cubic meta millioni 300 ambayo ni robo ya eneo la kisiwa cha palm limeshawahiwa.
Kutokana na ukubwa wa kisiwa cha Palm kisiwa kimegawanywa katika vieneo vidogo vidogo, eneo la kwanza ni eneo la kisiwa cha Deira. Eneo hili litakua kati ya dubai na bandari ya Al Hamriya. Kufikia mwezi wanne 2008 asilimia 80 ya ardhi ya Deira ilikua tayari imekamilika kujengwa. Muundo mpya wa muonekano wa deira ulipendekezwa na kutambulishwa mwezi wa kumi na moja 2008.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako