Wednesday 7 August 2013

UWANJA WA NDEGE, JOMO KENYATTA WAUNGUA LEO

Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) umefungwa kwa muda baada ya moto mkubwa kutokea katika uwanja huo mjini Nairobi, leo asubuhi.
Akielezea Mwandishi wa BBC amesema katika uwanja huo amesema kulikuwa na moshi mkubwa uliotoka katika eneo la kuondokea na kuingilia wageni.
Mamlaka ya uwanja huo imesema kuwa tayari watu waliokuwa katika eneo hilo wameondolewa katika eneo la tukio na kwa sasa moto huo umeweza kudhibitiwa.
Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta amewasili katika uwanja huo kuangalia hali halisi na anatarajiwa kuhutubia waandishi wa habari baadaye ili kuelezea mazingira ya Moto pamoja na hali ilivyo sasa.
Hadi sasa hakuna ripoti zozote ziliotolea kuhusu majeruhi kwenye tukio hilo wala mtu aliyepoteza maisha.
Akielezea msemaji wa uwanja huo wa ndege James Ole Lenku, amesema kuwa baadhi ya operesheni za uwanja huo zimekatizwa huku ndege zinazoingia katika uwanja huo zikielekezwa kutua katika viwanja vingine ndege kama vile Entebe, Dar es Salam, Kigali, Mombasa na kwingineko nchini Kenya. Baadhi ya safari za ndege kutoka uwanja huo wa ndege pia zimeahirishwa hadi hapo itakapoelezwa baadaye.
Mwishoni mwa wiki jana baadhi ya wenye maduka ya Duty Free katika uwanja huo walifurushwa baada ya serikali kusema kuwa leseni za wenye maduka zilikuwa zimepitwa na muda. 
Chanzo cha moto bado hakijabainika.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako