Sunday 18 August 2013

DKT. SLAA APOTEA NA HELIKOPTA ANGANI, ATUA KWA DHARULA

Katibu Mkuu wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dokta Willbroas Slaa

Katibu Mkuu wa Chama cha demokrasia na Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dokta Willbroad Slaa, jana alilazimika kutua kwa dharula na helikopta aliyokuwa akisafiria, baada ya kupotea akiwa angani kwa muda wa robo saa.
Rubani aliyekuwa akiendesha helikopta hiyo, alilazimika kutua kwa dharula baada ya kupotea eneo alilotakiwa kutua.
Tukio hilo lilitokea jana jioni wakati Dk. Slaa akitokea wilayani Korogwe akielekea Lushoto kwenye mkutano wa kuhamasisha kuunga mkono mapendekezo ya rasimu ya katiba mpya ambayo yanaungwa mkono na chama chake.
Dk. Slaa ambaye alikuwa atue Lushoto mjini, alipotea na kwenda kutua mji wa Mlalo katika wilaya hiyo ya Lushoto. Kutokana na tukio hilo, mkutano wake uliopangwa kufanyika katika wilaya ya Muheza ulichelewa kuanza.
Akihamasisha kuugwa mkono uwapo wa serikali tatu ambayo ni Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, alisema kuwa mfumo huo hauna gharama ikilinganishwa na serikali mbili za sasa.
Aliyasema hayo jana jioni katika uwanja wa Mavi, wilayani Muheza, alipohutubia maelfu ya wananchi wa Muheza.
Alisema kuwa serikali ya sasa ina gharama kubwa kwani ina wabunge wengi zaidi ya 438, wakiwamo wa Zanzibar na Tanzania bara na kulipwa mshahara mkubwa wa Sh. milioni 11 kwa mwezi.
Alisema zikiwapo serikali tatu, wabunge watapungua idadi na kubaki 314 kwani wabunge 124 watakuwa hawapo.
Alisisitiza Rais apunguziwe madaraka na pale anapokuwa madarakani au akimaliza muda wake, kisha ikabainika kuwa ametumia vibaya mamlaka yake akiwa Ikulu ashitakiwe.
Katika mkutano huo, Dk. Slaa aliongozana na mratibu wa ziara, Mwita Waitara na mjumbe wa kamati kuu Chadema Taifa, Mabere Marando.
Source: NIPASHE.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako