Saturday 3 August 2013

MILIONEA MDOGO WA KIAFRIKA ANAYEING'ARISHA TANZANIA




Milionea Patrick Ngowi alipigiwa simu na kupewa mihadi na mwandishi wa Jarida mashuhuri la FORBES, na mambo yalikuwa kama ifuatavyo.
 
 Patrick Ngowi, CEO, Helvetic Solar
Ni majira ya saa saba na Robo mchana siku ya Jumatano ndani ya Dar es salaam, Patrick Ngowi  amekaa kwa utulivu Regency Hotel ananisubiri tukutane kwa ajili ya mlo wa mchana, tulikubaliana kukutana saa sita na nusu mchana lakini nilichelewa.
“Hatimaye umefika kaka” Ngowi anatabasamu wakati anainuka kutoka kwenye kiti chake kunikaribisha.

Ngowi ni Mtanzania mwenye miaka 28 ambae amejenga kampuni ya solar energy yenye thamani ya dola millioni 8. Amevaa suti nyeusi ya kupendeza na amening’iniza peni kwenye mfuko wa suti yake, amevaa saa kwenye mkono wake wa kushoto mbayo imeendana na viatu alivyovaa.

Ngowi ana Historia ya kusisimua, Ni mkurugenzi mkuu wa Helvetic Solar Contractors kampuni ya kitanzania ambayo inasambaza, kuunda na kurekebisha mifumo ya Solar kaskazini mwa Tanzania, lakini cha kuvutia zaidi ni ukweli kwamba Ngowi amekua na mafanikio haya makubwa katika umri mdogo. Ngowi alianza kufanya biashara akiwa na umri wa miaka 15 wakati yupo shule na alikua akifanya biashara ya vocha za mitandao yote na wakati huo kulikua na wasambazaji wachache sana wa vocha kaskazini mwa Arusha ambapo ndio alipokuwa akiishi Ngowi upatikanaji wake ulikuwa ni mpaka kwenye Malls kubwa na Maduka ya simu hivyo Ngowi aligundua kuna tatizo hili la vocha kwa majirani zake akaamua kuwasaidia. Ngowi Alichukua  mtaji kwa mama yake kiasi cha shilingi elfu hamsini akanunua vocha za jumla kwa ajili ya kuwauzia watu, Ngowi alikuwa bado anasoma hivyo hakupata muda mwingi wa kufanya biashara yake na kuamua kuwapa wauzaji wa sheli wamsaidie kuuza vocha kipindi ambacho yupo shuleni.



“Ilikua sio biashara kubwa” anasema Ngowi, lakini nilipenda ukweli kwamba nilikua natengeza hela na hivyo nikawa najitegemea kwa kiasi kidogo. Mafanikio makubwa niliyoyapata saivi yametokana na kazi niliyokuwa naifanya kipindi cha nyuma. Nilijifunza kuhusu faida na hasara, kutawala soko na kuajiri watu sahihi katika biashara kwa kifupi nilijifunza vitu vingi”

Alipomaliza elimu ya sekondari, Ngowi alikaa nyumbani mwaka mmoja kabla ya kujiunga na elimu ya chuo. Kipindi hicho simu za mkononi zilikua ni chache na gharama sana kwa kijana kama yeye kumiliki na ndo kipindi ambacho alifanya ziara ya kwenda Asia ambako aligundua kuna simu za bei ya chini aliamua kuchukua mkopo kwa mama yake kiasi cha dola 1800 na kuanza kufanya safari rasmi kati ya Tanzania na Hongkong kununua simu za mkononi kwa watengenezaji wa gharama za chini na kuziuza kwa wasambazaji wa simu wa Tanzania.

“Nilikuwa natengeneza kiasi kikubwa cha hela na kipindi hicho nilikuwa na umri wa miaka 18 na miezi sita tu lakini nilikuwa natengeneza kiasi cha dola 150, 000, maisha yalikuwa mazuri. Kutokana na safari zake za mara kwa mara kwenda Hongkong na China Ngowi aligundua nishati ya Jua na akajifunza kuhusu matumizi ya nguvu ya jua kwa mara ya kwanza.

Tanzania ina tatizo kubwa la nguvu kazi kwenye miundombinu mbalimbali, kipindi cha safari za Ngowi mara kwa mara kwenda Asia nguvu ya umeme Tanzania kwa ajili ya kutendea kazi mbalimbali na matumizi ya nyumbani ilikuwa 10%. 

Kampuni nyingi, asasi za kiserikali na familia zenye kipato kikubwa zilitegemea sana nguvu ya jenereta. “Tatizo la umeme Tanzania lilikua kubwa na nikafikiria kuwa Tanzania itakuwa inahitaji nguvu ya umeme ya ziada, aliongea Ngowi huku akiinua kinywaji chake.

Kulikuwa na bahati na Ngowi alitaka kuitumia lakini wazazi wake walisisitiza kwamba amalize kwanza elimu yake. Ngowi anatokea kwenye familia ya wasomi. Wazazi wake wote ni wakufuzi.

“kuanzia nimeanza biashara ya vocha mama yangu aliniambia nihitimu kwanza masomo yangu, “kuacha shule sio chaguo langu, aliniweka wazi kuanzia mwanzoni” aliongea Ngowi. Akiwa na miaka 19 Ngowi aliacha kufanya biashara na akaendelea na masomo yake . alikuwa tayari ameshavutiwa na nguvu ya mionzi ya jua China hivyo alienda kusoma China chuo kikuu cha Denzhou ambako alisomea nguvu ya umeme ya kutengenezwa. Ilikuwa ni ndoa sahihi kwani alikua ameipenda china na akawa mdadisi kuhusu nguvu ya mionzi na mafanikio ambayo inaweza kuyaleta kwa watu.


Wakati yupo Denzhou Ngowi alianza biashara isiyo rasmi ya kusafirisha bidhaa nje ya nchi kwani tayari alikuwa na uhusiano na baadhi ya viwanda vya ujenzi kwahiyo alikuwa na oda kutoka kwao. “Hivyo ndio namna nilivyoweza kutengeneza mtaji wa biashara nzima”

Mpaka muda aliomaliza masomo yake, Ngowi alikuwa na mtaji wa kutosha, akaandaa vifaa vya kusaidia kutengeneza umeme wa mionzi alipomaliza tu degree yake akarudi Arusha kuanzisha biashara yake mwenyewe.

“Ghala ya kwanza kuifungua ilikuwa ndogo lakini ilikuwa katika eneo zuri. Tulijitangaza sana hasa kwenye shule, serikali, hospital na wengine waliopenda kutumia nishati hii” Ngowi akaelezea

Haikuwa rahisi wakati tunaanza, nishati ya jua haikuwa maarufu sana kwa watanzania hivyo biashara haikwenda haraka kama tulivyodhani.

“Miezi ya mwanzo mauzo yalikwenda taratibu” namshukuru mama kwa kuwa alinipa nguvu ya kuendelea na biashara, kwa maneno yake ya kunitia moyo.



Kuna wakati nilikuwa nadhani nimeingia kwenye biashara mbaya na kufikiri nitafeli lakini mama alinishauri kuendelea, wakati mwingine ni muhimu kuwa na mtu anayeamini unachofanya.

Ngowi aliendelea na kuitangaza biashara yake kwa yeyote aliyefikiria atahitaji, na baada ya vituo vya habari kupigia kampeni nishati mbadala hapo ndipo biashara ilipoanza kushika kasi.

Kampuni yake, Helvetic Solar ni kampuni pekee iliyopo Arusha inayotoa nishati mbadala ya umeme wa jua. “yeyote anayehitaji nishati ya jua lazima aje kwetu, wapinzani wengine wapo Dar es Salaam ambapo ni mbali kwa hiyo soko la Arusha lote la kwetu.

Biashara ilianza kuwa nzuri kwa Ngowi mwaka 2007, ambapo kampuni ilianza kuwawekea nishati ya jua wateja wadogo wadogo na wateja wakaanza kupeana taarifa pamoja na mawasiliano, ghafla mawakala wa serikali nao wakaanza kututafuta tuwawekee nishati ya jua pamoja na kampuni zingine nyingi.
 Mafanikio yakaanza kuonekana mwaka 2011 ambapo mapato yalifikia Dolla za kimarekani milioni 2.8, na mwaka 2012 dola milioni 6.8 na mwaka huu inakadiliwa mapato yatafikia dola milioni 10.

Wateja wakubwa wa kampuni ya Helvetic’s ni pamoja na Umoja wa Mataifa, Jeshi la Tanzania, Shirika la WorldVision, na kanisa la Kilutherani pamoja na wengine wengi.

Ngowi anampango wa kupanua kampuni yake kimataifa na ameshaanza kusambaza nishati hiyo ya jua kwa baadhi ya taasisi za kuserikali za Rwanda “Ni furuha kwetu tumeanza kupata wateja kutoka nchi za jirani, wanapenda huduma zetu kutokana na historia nzuri walizonazo na ubora wa bidhaa zetu,, hivyo kupata mikataba mbalimbali,” Ngowi anaelezea

Pia Ngowi ameweka mkataba wa takribani Dola million 5, na kampuni za utalii (Hotel na maeneo ya kufikia wageni) mkoani Arusha

Kampuni ya KPMG Mashariki mwa Africa imeitaja Helvetic Solar kama kampuni namba moja inayokuwa kwa kasi katika mapitio ya kampuni 110 boranchini Tanzania kwa mwaka 2012 – 2013. Pia Ngowi yumo kati ya wagombea tuzo ya Kijana mdogo wa Kiafrika mwenye mafanikio inayotolewa kila mwaka na Nobel.

Ngowi amekutana na changamoto nyingi hadi kufikia hapo katika biashara yake

“natamani kuwa na Bank moja ambayo itanihakikishia mikopo kulingana na mikataba ninayopata, ila ni ngumu sana lingine ni miundombinu pamoja na fikra, ninafanya kazi za umeme ambazo zinahitaji ubunifu kila mara, wakati mwingine kupata miundombinu inakuwa ngumu hiyo inabidi niagize kutoka nje.”Anaongezea Ngowi

Changamoto ingine aliyonayo Ngowi ni mipango yake ya kukuza mtaji wa kampuni yake kuingiza mapato zaidi ya Dola milioni 100 ndani ya miaka mitano ijayo.

Ngowi, Muumini wa Dini ya Kikristo ambaye anaamini sana imani yake ambayo inamuhakikishia ya kuwa hakuna linaloshindikana chini ya jua, “ kama mungu kanifikisha hapa, ninajua atanipeleka pale ninapofikiria kufika” anamalizia Ngowi.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako