Sunday 11 August 2013

ARSENAL WAITANDIKA MANCHESTER CITY 3-1


KLABU ya Arsenal jioni ya jana imeizabua Manchester City kwa mabao 3-1 katika pambano lililofanyika  kwenye Uwanja wa Olimpiki mjini Helsinki ukiwa ni mchezo wa kirafiki.
Arsenal inayohaha kumsaka mshambuliaji wa Liverpool, Luis Suarez, walipata mabao yao kupitia kwa Theo Walcott dk ya 9, Aaron Ramsey dk 59 na Olivier Giroud dk 62.
Bao la kufutia machozi la City liliwekwa kimiani 'jioni' kabisa na Negredo dk 80.
Nayo Liverpool imejikuta ikiwashwa bao 1-0 na Celtic ya Scotland huku Tottenham ikitoshana nguvu na Espaniol katika mechi zingine za kirafiki zilizochezwa leo.


No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako