Sunday 4 August 2013

MTANZANIA ASHINDA MASHINDANO YA KURUKA KAMBA MAREKANI

Bingwa wa dunia wa kuruka kamba akionyesha medali pamoja na kombe zawadi alizopata kwa ushindi huko Marekani.
Hamis Mohamed na wenzake wakionyesha umahiri wao wa kuruka kamba ndani ya Ikulu jana jioni.
 Rais Kikwete akitizama medali ambazo Hamis Mohamed ameshinda kutokana na mchezo wa kuruka kamba.

Rais Kikwete akimpongeza Hamis Mohamed kwa kutwaa ubingwa wa dunia na kuipa sifa Tanzania ambayo kwa miaka mingi haijashinda medali yeyote katika michezo ya kimataifa.
Kijana Hamis Mohamed na wenzake jana jioni walialikwa na Rais wa Tanzania, Rais Kikwete kupewa pongezi baada ya kushinda ubingwa wa dunia katika mchezo wa kuruka kamba, mashindano yaliyofanyika hivi karibuni Nchini Marekani.
Akimuelezea kijana Hamis Mwenyekiti wa Sport Training Centre (TSTF), bwana Dennis Makoi amesema kuwa walipotambua kuwa kijana huyo ana kipaji cha mchezo huo waliamua kumtafuta mfadhili ili kukiendeleza kipaji chake. Aliongeza kuwa walipata mfadhili kutoka Marekani ambaye anamiliki kituo cha kufundishia mchezo huo ambaye alimchukua Hamisi kwenda Marekani Desemba mwaka jana kwa ajili ya kuendeleza mafunzo kwa kijana huyo.
Makoi aliendelea kusema kijana huyo akiwa katika kituo cha mfadhili huyo alishiriki mashindano ya dunia ya mchezo wa kuruka kamba yaliyofanyika Julai 5 hadi 13 mwaka huu jijini Orlando, Marekani ambapo yalishirikisha washiriki 480 kutoka timu 44 kwenye nchi 14 na Tanzania ilitoa jumla ya wachezaji 6 akiwemo Hamis aliyeongoza na kunyakua kombe hilo.
Amy Canady ambaye ndiye alimchukua na kumfadhili kijana Hamis alisema kuwa amefurahishwa na jitihada za kijana huyo ambapo anafaa kuwa mfano na kupewa usimamizi mkubwa, pia amesema lengo lao ni kujenga kituo cha mchezo huo Tanzania ili kuukuza ambapo vijana watapata fursa ya kucheza wakiwa nchini kwao na kuitangaza vyema Tanzania.
Hamisi mwenyewe alisema anashukuru kwa malezi aliyoyapata katika kituo cha watoto yatima cha Dogodogo Centre na kwa msaada waliojitolea katika kuendeleza kipaji chake. 

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako