Tuesday 27 August 2013

MTU ANAYEONGOZA KWA KUWA NA TATOO NYINGI MWILINI

'Human branding' ambayo inajulikana pia kama 'scarification', ndo kitu kinachoongoza sasa hivi kwenye sanaa ya kujichora mwilini na mwingereza mwenye tatoo nyingi kuliko wote hakutaka kuachwa nyuma na style hiyo mpya. 
Matthew Whelan,33, kutoka Birmingham hajajifunika mwili wake kutoka kichwani hadi vidole vya miguuni  tu na sanaa ya ngozi bali hadi jicho lake moja jeupe kaliweka tatoo na kuwa jeusi. Hicho kifaa kilichotumika kumchora tatoo kinatumia nguvu ya umeme kuunguza kwenye nyama  na ndio kifaa hicho hicho kinatumika na madaktari wa meno au surgeons kuunguza seli za kansa.
Lest Westwood, mchora tatoo aliyemchora alisema "Huwa inanukisha studio yote mwili wake unapoungua na kuna hatari pia ambazo zinaambatana na kujichora tatoo hivi, mwili unaweza ukapata shock".
Bwana Whelan alikua na miaka 9 tu alipoanza kutamani sana tattoo na tangia hapo alitumia masaa 300 kwenye kiti cha wachora tatoo na alitumia zaidi ya euro 20,000 kujipamba mwili wake.
Designs zake zilitoka kwenye maumbo ya nyoka, ng'e(scorpions) na binadamu wa kutisha (vampires) hadi jina la TV program anayoipenda sana ‘The Jeremy Kyle Show’ alijichora tatoo ya kipindi hicho kwenye kisogo chake. 
Hapo hapo, Whelan ambaye amebadilisha jina lake kisheria na kujiita 'His Royal Majesty Body Art, King of Ink Land' alisema anapenda kujifikiria kuwa yeye ni kipande cha sanaa kinachopumua na kuishi.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako