Friday 7 June 2013

YANGA USHIRIKI CECAFA DARFUL, UTATA




 

HABARI zilizotufikia hivi punde kutoka katika mtandao mmoja wa kimichezo nchini umemnukuu mmoja wa watu wa karibu wa klabu ya soka ya Dar es salaam Young Africans akithibitisha kuwa klabu hiyo haitashiriki michuano ya kagame itakayoandaliwa katika jimbo la Darfur nchini SUDAN.

Hatua hiyo imekuja kufuatia tamko la waziri  anayehusika na mambo ya nje nchini Mh Bernard Membe aliyotangaza bungeni kuwa jimbo la Darfur linalotarajiwa kuwa miongoni mwa sehemu zitakazochezwa michuano hiyo hazina usalama, na wageni wanaofika huko huvishawa flana zinazozuia risasi(Bullet proof) kwa ajili ya usalama wao.

 Pia Waziri huyo alitanabaisha kutokuwepo kwa hoteli zenye hadhi ya kupokea wageni na kuzishangaa timu zinazojiandaa kuelekea huko.

Tayari vilabu vikubwa vyenye ushawishi katika ligi hiyo vimeshatangaza kutopeleka timu katika jimbo hilo DARFUR  SIMBA YA TANZANIA, TUSKER YA KENYA,AL HILAL  NA EL- MEREIKH ZOTE ZA SUDAN KUSIN,
Mashindano ya kagame huandaliwa kila mwaka yakijumuisha vilabu bingwa vya ukanda wa Afrika mashariki na kati na Dar es salaam Young Africans ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako