Sunday 9 June 2013

TAIFA STARS YAFA KIUME MORROCCO.

 kikosi cha Timu ya taifa ya Tanzania Taaifa stars
TIMU ya soka ya Tanzania imeshindwa kutamba mbele ya miamba ya Afica ya kaskazini Morocco kwa kufungwa magoli 2-1, Katika mchezo mulioanza majira ya saa tano kwa saa za Africa Mashariki.
Dakika ya 18, almanusura Thomas ulimwengu aipatie bao Stars mara baada ya kuaambaa amba na mpira  akipokea pasi ndefu kutoka kwa nyota wa mchezo kwa upande wa stars Amri Kiemba lakini Ulimwengu alipioga shuti mtoto lililodakwa na golikipa wa Morocco.
Moroccco walipata goli  kwa penati dakika ya 28  kufuatia beki wa timu ya taifa ya Tanzania Agrey Moris kumsukuma mshambuliaji wa Morocco aliyekuwa amebaki yeye na mlinda mlango wa Tanzania Juma Kaseja na kupelekea kuzaa goli la kwanza lililodumu hadi mapunziko.
Kama hiyo haitoshi Mwamuzi wa mchezo huo alimzawadia kadi nyekund mlinzi huyo na kufanya Stars kucheza wakiwa pungufu kwa karibia muda wote.
Goli la Taia stars lilikwamishwa kimiani na kiungo Amri Kiemba kwa shuti kali la umbali wa zaidi ya mita 30
Katika mchezo huo stars ilifanya mabadiliko kwa kumtoa Mrisho Ngassa na Nafasi Yake Kuchukuliwa Na Nadir Haroub Canavaro kuziba pengo la Moris aliyetolewa kwa kadi nyekundu, na Thomas ulimwengu nasi yake kuchukuliwa na Hamis Mcha.
John Bocco "Adebayo" aliiingia mnamo dakika ya 95 akichukua naasi ya Hamis Mcha aliyeonekana kupotea mchezoni.

FAILASUFA & DOX DANTA

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako