Saturday 8 June 2013

MAZISHI YA MUME WA KHADIJA KOPA, MAREHEMU JAFARI ALLY

Waumini wa Kiislam wakiuswalia Mwili wa Marehemu Jafari Ally Nje ya Nyumba yake, Bagamoyo jana Mchana
Wakazi wa Bagamoyo wakibeba Mwili wa Marehemu Jafari Ally kwenda Makaburini

Mume wa mwimbaji wa muziki wa taarabu hapa nchini, Khadija Kopa, ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Magomeni, Jafari Ally, amezikwa jana Majira ya saa Saba na nusu, katika makaburi yaliyopo mjini Bagamoyo
Msiba wa Ally umehidhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo Waziri wa Elimu naMafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa, Mtoto wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ridhiwan Kikwete na viongozi wengine mbalimbali wa CCM.

Akizungumza kwa machungu makubwa, Malkia wa Mipasho Khadija Kopa, alisema amejisikia uchungu mume wake kufariki huku akiwa nje ya jiji la Dar es Salaam, huku akirejea akimkuta mumewe ni marehemu.
 Alisema kuwa msiba wa mumewe umempa uchungu mkubwa, huku akiamini kuwa utaendelea kuwa kichwani mwake kwasababu ya kuondokewa na mume wake aliyempenda.
 “Nimeumia sana na msiba huu wa mume wangu,” alisema Khadija Kopa, huku akibubujikwa na machozi.
 Naye, Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Bagamoyo, Shukuru Mbato, alitumia muda mwingi kuwataka Watanzania wakiwamo wakazi wa Bagamoyo kuishi kwa upendo sambamba na kumuombea marehemu aishi kwa amani katika maisha yake mapya.
 “Sisi tulimpenda sana, ila Mungu ndio muweza wa yote, hivyo sisi kama binadamu lazima tukubali matokeo,” alisema Mbato.

Marehemu Jafari Ally alifariki Dunia Juzi alfajiri katika Hospital ya Lugalo Jijini Dar es Salaam kwa ugonjwa wa Kifua.
Inna Lilah wainalilah Rajiun

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako