Thursday 13 June 2013

KIKONGWE KIMURA AFARIKI DUNIA

Kikongwe, Jiroemon Kimura akisherehekea umri wa miaka 116 katika nyumba yake mjini Kyotango-Japan Photo: AFP/Getty Images
Jiroemon Kimura, amezaliwa mwaka 1897, kafariki hospitalini mapema Jumatano na kifo chake kutangazwa na serikali ya Japan.
Bwana Kimura, kutoka Kyotango - Kyoto Prefecture, ndiye aliyekuwa akishikilia rekodi ya kuishi umri mrefu kuliko binadamu wengine kwa mujibu wa Kitabu cha kumbukumbu duniani cha Guinness kilichotolewa Desemba, 2012 na alifariki akiwa na umri wa miaka 115.
Mnamo tarehe 28 mwezi Desemba alivunja rekodi ya Bwana Kimura kwa kutimiza umri wa miaka 115 na siku 253.
Hatahivyo, binadamu anayeshikilia rekodi ya kuishi umri mrefu kuliko wote kutokana na rekodi zilizopo ni mwanamama wa Kifaransa, Jeanne Calment, aliyefariki mwaka 1997 akiwa na umri wa miaka 122. (Lakini kuna Mtanzania Mzee Kitwala alifariki mwaka 1992 akiwa na umri wa miaka 125, pia Mnepal Bir Narayan Chaudhary, aliyefariki mwaka 1998 inasadikiwa alifarika akiwa na umri wa miaka 141, japo hawa wote hawatambuliwi na kitabu cha kumbukumbu GUINESS kwa kuwa hawana vyeti vya kuzaliwa)
Bwana Kimura, alizaliwa mwaka 1897 Nchini Marekani alisherehekea miaka 116 ya kuzaliwa mwezi wa nne (April) mwaka huu na kupatiwa zawadi na Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe.
Wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya kutimiza miaka 116 Bwana Kimura alitembelewa na wazee zaidi ya 100 wenye umri zaidi ya miaka 100 ili kumpa moyo wa kuishi miaka mingi zaidi.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako