Friday 4 October 2013

MTOTO ALIWA NA FISI BAADA YA KUGONGWA NA KUTUPWA PORINI

Katika hali ya kusikitisha na ya ukali wa hali ya juu dereva bodaboda aliyefahamika kwa jina moja la Mbikano anasakwa na jeshi la polisi Mkoani Mtwara kwa kusababisha mauaji ya mtoto mdogo ambae alimgonga wakati akiendesha bodaboda yake na kumuumiza mguu kisha akambeba na kukimbia nae na baadae kumtupa kwenye kichaka na fisi wakaja kumla na kubakisha fuvu
Habari za uhakika zilizonaswa na mwandishi wa Xdeejayz aliyeko Masasi na Mtwara zilisema tukio hilo la kusikitisha limewaliza watu wengi, akiongea na xdeejayz kwenye mahojiano maalum mjomba wa mtoto huyo aliyejitambulisha kwa jina la Mjomba wa mrehemu Yusuph Hashim (30) alisema tukio hilo lilitokea  tarehe 29 Septemba, 2013 majira ya saa 12:30 jioni.
Mjomba huyo aliendelea kueleza kuwa siku hiyo mtoto huyo aliyeitwa kwa jina la Shabiru Muhidin (4) ambapo wanaishi katika Kijiji Mkaseka wote na mtoto huyo muda huo alikuwa ametumwa dukani na mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Thawabu Hakhim Nakanje.

Hata hivyo katika ha ilisiyotajia mjomba huyo alisema kuna kundi la vijana waliokuwa wanatoka kwenye kutizama mpira kwenye kijiji cha Jirani  cha Mkururu huku wakiwa wamepakizana kwenye bodaboda walivyofika maeneo ya Mkaseka ndipo walipomgonga mtoto huyo na kumjeruhi mguuni na walipoona watu wameanza kujaa ndipo walipomchukua mtoto huyo ambae alikuwa akilia kwa uchungu na kuondoka nae kusikojulikana.
Mjomba huyo aliendelea kuileza xdeejayz kuwa kijana huyo aliyekuwa anaendesha bodaboda aliendelea kutokomea kizani na mtoto huyo hadi alipofika mahali penye msitu mkubwa alimrusha kichakani huku mtoto huyo alimsihi asimuache msituni hapo kwani angeliwa na wanyama lakini bila huruma dereva huyo wala hakujali hatimaye alimuacha mtoto huyo.
Habari zaidi ziliendelea kusema huku nyuma alipogongewa mtoto habari zilianza kusambaa ambapo mjomba huyo alipopata taarifa hizo aliondoka na majirani zake kuelekea kwenye zahanati ya kijiji hicho kwa kudhani huenda watu hao waliamua kufanya ubinadamu kwa kumpelekea hospitali baada ya kumuumiza ambapo alipofika kwenye zahanati hiyo hakumkuta mtoto huyo.
Baada ya kumkosa kwenye zahanati hiyo walienda kwenye kituo kikubwa cha Afya cha Nagaga lakini hapo napo hawamkuta ndipo walishauriana kwenda kuripoti kwa mkuu wa polisi jamii na mara baada ya kukutana na kamanda wa polisi jamii aliyefahamika kwa jina la Hamis na baada ya kuwasikiliza aliitisha kikao cha dharula na wakaanza kumtafuta mtoto huyo hapo ilishakuwa siku iliyofuata ambapo baada ya msako kufanyika walienda hadi kwenye sehemu moja yenye kilima msitu.
Baada ya kufika kwenye mlima huo waliona mburuzo ulioambatana na damu na walipoenda mbele zaidi waliona damu nyingi zikiwa na vimetapakaa na vipande vya utumbo na fuvu kipande kidogo tu hali waliyogundua kuwa mtoto huyo alishapoteza uhai wake kwa kuliwa na fisi ambao eneo hilo wako wengi kama mbuzi.
Kufuatia kushuhudia hayo kamanda wa ulinzi shirikishi alipiga simu kituo cha polisi Masasi ambapo polisi walifika haraka na kupiga picha eneo la tukio huku wakiondoka na mabaki ya fuvu hilo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Hata hivyo hadi sasa mmiliki wa bodaboda hiyo anashikiriwa na jeshi la polisi huku mtuhumiwa namba moja akitafutwa kwa udi na uvumba ili kufikishwa mbele ya mkono wa dola.
Xdeejayz ilifanya jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi Mkoa wa Mtwara  ili kuzungumzia ambapo baada ya kupigiwa simu ilipokelewa na mlinzi wake huku akisema kuwa Kamanda yuko bize na vikao hivyo atafutwe jioni ya leo.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako