Wednesday 29 January 2014

RONADINHO GAUCHO AHAMIA KWENYE MUZIKI

Mara nyingi inazoeleka kwa Star yoyote duniani kufanya kitu kilichosababisha awe star, yaani kama muimbaji atajitahidi kukomaa na uimbaji, kama ni mchezaji mpira atajitahidi kukomaa na mpira, japo kwa sasa tunawashuhudia wasanii wengi wa movie kwa Tanzania wakijaribu muziki na baadhi yao kupokelewa vizuri.
Miongoni mwa wasanii wa Tanzania waliopokelewa vizuri wakitokea kiwanda cha Movie Tanzania kuna Shilole, Snura, Kitale, Baby Madaha, Marehemu Sharo Milionea na wengine wengi.
Kwa hapa nataka tumzungumzie Mwanasoka maarufu kutoka Brazil Ronadinho Gaucho ambaye ameonekana ana vipaji vingi mara baada ya kuonekana kwa video hii akiimba, nyimbo hii inahusu wale waliokata tamaa ya maisha.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako