Monday 23 September 2013

WATU ZAIDI YA 59 WAUWAWA KENYA



Vikosi vya Kenya vimezidi kuongezwa kwenye eneo la maduka la westgate, Nairobi ambapo watu wanaodhaniwa kuwa ni Al-shabab wameendelea kulishika jengo hilo na mateka kadhaa.
Hadi sasa watu wapatao 59 wameripotiwa kuuwawa na wengine 175 kujeruhiwa huku kukiwa hakuna idadi maalum ya mateka waliokwama ndani ya jengo hilo.
Al-shabab wametuma ujumbe kwenye akaunti yao ya Twittwer wakithibitisha kuhusika na tukio hilo, huku wakisifia kuwa vijana wao bado wameweza kulishikilia jingo hilo kwa masaa 20 sasa.
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameomba umoja kwa raia wa nchi hiyo katika kipindi hiki kigumu na kusisitiza kuwa wahusika wa tukio hilo watakamatwa popote walipo iwe ni ndani ya nchi ama nje ya nchi hiyo.
Tayari nchi kadhaa zimethibitisha kupoteza raia wao katika tukio hilo.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameliita shambulizi hilo ni la kiwoga. Imeripotiwa kuwa raia wawili wa ufaransa ni miongoni mwa waliokufa.
Wakati Marekani ikidai kuwa ina raia wake kadhaa waliojeruhiwa katika tukio hilo, Kanada wao wamepoteza raia wawili nao.
Baraza la usalama la umoja wa mataifa limelaani tukio hilo kwa kauli kali na kuitahadharisha Kenya kuwa juhudi zozote za kutatua tatizo hilo ni lazima zizingatie haki za Binadamu.
Kenya imekumbwa na mashambulizi madogo madogo ya kutumia mabomu ya kurusha kwa mkono tangu ilipoingiza jeshi lake nchini Somalia kupambana na Al-shabab mwishoni mwa 2011, ambapo kundi hilo linapigana na serikali ya Somalia kuweza kusimamisha sharia za kiislaam.
BY: www.habarika.info

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako