Monday 2 September 2013

BALE ATAMBULISHWA RASMI REAL MADRID


 
Klabu ya Real Madrid imevunja mzizi wa fitina baada ya jana kumalizana na kiungo mshambuliaji, Gareth Bale kutoka Tottenham Hotspur kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya pauni 100 milioni.
 

Mchezaji huyo raia wa Wales amevunja rekodi ya mchezaji mwenzake wa timu hiyo,  Cristiano Ronaldo a mbaye alisajiliwa kwa ada ya uhamisho ya pauni 80 milioni mwaka 2009, hivyo kufanya timu hiyo kuwa na wachezaji waliosajiliwa kwa gharama kubwa.
“Napenda kuwashukuru kila mtu katika klabu yangu, Mwenyekiti,  bodi, wafanyakazi wote, kocha na wachezaji wenzangu na zaidi mashabiki ambao naamini watanielewa kwa maamuzi ytangu ya ajabu ya kumaliza maisha yangu katika klabu yangu," alisema Bale alipokuwa anazungumza na tovuti ya Tottenham.

“Nina uhakika kuwa huu ni wakati mzuri kuondoka katika ambayo nilikaa vizuri na kucheza soka zuri katika siku zote zilizokuwa pale. Najua wachezaji wengi wanapenda kujiunga na klabu bora yenye wachezaji wenye vipaji, lakini ninachoweza kusema, ndoto yangu imetimia.

“Pamoja na kuondoka lakini Tottenham ipo moyoni mwangu wakati wowote na nina uhakika msimu huu utakuwa wa mafanikio kwao. Sasa naangalia mbele, kinachofuata katika maisha yangu ni kucheza soka katika klabu ya Real Madrid.”

Wakati Madrid wakikamilisha kumnunua Bale wamemruhusu kiungo wake, Kaka kutua katika klabu ya AC Milan ya Italia. Madrid walikubaliana na Milan lakini walikuwa wakisubiri kukamilisha usajili wa Bale.
STORY BY: MASALU JR

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako