Friday 22 November 2013

MWANAMKE ALALA NA MAITI YA MUME WAKE KWA MWAKA MMOJA KATIKA KITANDA KIMOJA


Inakuwa ni jambo gumu sana kuliamini hasa kabla haujatazama ni nini kilicho tokea wakati huo  2012, ambapo mwanamke mmoja aliamua kulala na maiti ya mume wake katika kitanda kimoja kwa kipindi kinacho dhaniwa kuwa kilikuwa ni mwaka mmoja.  
Mwanaume huyo marehemu  Marcel H, 79 alifariki mwezi wa kumi na moja mwaka jana katika nyumba za kupanga za Brussels ambapo kifo chake kilisababishwa na ugonjwa wa Asthma, na mke wake mpenzi aliyekuwa na miaka 69 ambaye jina lake halikutajwa aliamua aendelee kukaa nae kwa kipindi chote hicho bila hata kujali harufu mbaya ambayo ilikuwa ikuitoka.
hata hivyo majirani hawakuweza kutambua swala hilo kwamba yule mama alikuwa akilala na maiti ndani ya nyumba hiyo hadi ilipokuja kugundulika kwa sababu mwenye nyumba alikuwa akidai kodi yake ya mwaka , baada ya kuingia ndani ya nyumba ndipo alipo gundua hayo... sasa hivi ndivyo ilivyo kuwa
Tazama maiti hii ilivyo kuwa imeoza, mbaya zaidi kulikuwa na baadhi ya majimaji kutoka katika mwili huu ambao ulisababisha harufu mbaya sana lakini bado mama huyu alikuwa akilala na maiti hii bila kujali, pia kulikuwa na wadudu hatari ambao wanapatikana katika mwili ulio oza kama funza lakini mama huyu alikuwa hata hajali...


No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako