Wednesday 4 February 2015

YANGA VS COASTAL UNION



 Kilabu ya Dar YOUNG African yenye makazi yake mitaa ya Jangwani imewasili Jijini Tanga tayari kukipiga na coast union katika mchezo wa ligi kuu Vodacom Tanzania bara

Lakini Yanga wamekataa kufanya mazoezi kwenye Uwanja wa Mkwakwani ambao walitakiwa kufanya mazoezi pindi walipofika na kuamua kufanya mazoezi kwenye uwanja wa jeshi.

Msemaji wa Yanga, Jerry Muro amesema walipanga kufanya mazoezi kwenye uwanja huo na si Mkwakwani.

“Nafikiri hakuna tatizo, kilichotakiwa pale ni suala la mazoezi na tumefanya, hivyo hakuna tatizo lolote,” alisema Muro.

Yanga ipo uwanjani kuvaa na Wagosi wa Kaya Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga
Wadau wa soka wanaizungumzia mechi hii ni kama Yanga na SIMBA


No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako