Thursday 5 February 2015

GERRARD ACHEZA MECHI YA MIA 7 WAKATI LIVERPOOL WAKIIUA BOLTON 2 - 1



LIVERPOOL imetinga Raundi ya Tano ya Kombe la FA baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Bolton Wanderers  hapo jana.

Eidur Gudjohsen aliifungia Bolton bao la kuongoza kwa  mkwaju wa penalti dakika ya 59, baada ya kinda wa miaka 19, Zach Clough kuchezewa vibaya na beki wa Liverpool, Martin Skrtel ndani ya 18

Raheem Sterling akaisawazishia Liverpool dakika ya 85, kabla ya Philippe Coutinho kufunga goli la ushindi dakika ya 90. 

KIUNGO Steven Gerrard amekuwa mchezaji wa tatu wa Liverpool kutimiza mechi 700 kihistoria baada ya kuichezea timu hiyo jana ikishinda 2-1 dhidi ya Bolton katika mechi ya marudio Raundi ya Nne ya Kombe la FA.
Gerrard, ambaye maisha yae yote amecheza Liverpool pekee, alifurahia mafanikio yake hayo kwa kuvaa kiatu maalum kilichoandikwa 700 nyuma pamoja na majina ya mabinti zake, Lilly na Lexie.

Bolton ililazimika kucheza pungufu kwa dakika 20 za mwisho baada ya mchezaji wake, Neil Danns kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na Liverpool sasa itamenyana na Crystal Palace katika Raundi ya Tano.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako