Tuesday 13 January 2015

CHRISTIANO RONALDO MCHEZAJI BORA WA DUNIA FIFA BALLON D' OR KWA MARA YA 3 SASA

C 7


Christiano Ronaldo ndiye mshindi wa tuzo ya mwanasoka bora Ulaya na Duniani kote maarufu kama Ballon d'Or.
Ronaldo mwenye miaka 29, ametwaa tuzo hiyo kwa kumbwaga mpinzani wake mkubwa Lionel Messi wa Barcelona na kipa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Raia huyo wa Ureno ametwaa tuzo hiyo kwa mara ya pili mfululizo hii ikiwa ni mara yake ya tatu kutwaa tunzo hiyo kwa kuwa mara ya kwanza aliibeba 2008 akiwa na Manchester United.

Mwaka jana, Ronaldo akiwa na Real Madrid aliiwezesha kutwaa ubingwa wa Ulaya, Copa del Rey, Uefa Super Cup, pia ubingwa wa dunia huku yeye akifunga mabao 56 katika mechi 51.

Dakika chache baada ya kutwaa tuzo ya mchazaji bora wa dunia, Cristiano Ronaldo amefunguka wazi kwamba anataka kumfikia mpinzani wake Lionel Messi.


Ronaldo ameeleza kufurahishwa kwake na kutwaa tuzo yake ya tatu lakini akasisitiza angefurahi kuichukua kwa mara ya nne kama ilivyo kwa lionel Messi.

No comments:

Post a Comment

Ahsante kwa Maoni yako