Mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi hauzwi na klabu hiyo inapanga kujadili mkataba mpya na raia huyo wa Argentina, amesema rais wa klabu hiyo Joseph Maria Bartomeu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJAEZUK7eejw4k6Pts_ajLuwrZDkoCoboWGSBsV7y5BCZh2BSQWttMfXTsdxCP9Vc0N6BhHFlHXgHE_161dJ2T5JNkUmQZkZ0ZyZgHpiljO0U7Dmktytevp91uOCUMeV_ge2-CPfMFf0o/s1600/Messii.patapicha.jpg)
Kuna uvumi kuwa Messi ambaye ni mshindi mara nne wa tuzo la Ballo d’Or, mwenye umri wa miaka 26, anatakiwa na matajiri wa klabu ya Ufaransa ya Paris St-Germain.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjdJWFk5xH1-8XqMRRbuq6OpN9b6_VPpzOEvZkzM5EVyC2hyYhY8Z-oq1_UyWGyoAOMu5gxdeEAbNqeSbDgLqvJ621oXREf3xT8AoRfBRTdbZRlYMxBxqZBlLrynOrY0zMFpwSf6dpgc7A/s1600/Messi.patapicha.jpg)
Katika mahojiano na kituo cha radio cha RAC1, yaliyonukuliwa katika mtandao wa Barcelona, Bartomeu anasema: “Klabu itakaa na kuangalia mkataba mpya. Tutafanya kila tunaloweza kuhakikisha kuwa yeye ndiye mchezaji anayelipwa mshahara bora zaidi duniani.”
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcS-vqdz-vvt76dinvudX4_K5A-9gewPx4qXXz6r-JCkF9NguWfVlWV2eQLl99Z00U_9_GTgJ1YQqhHJ5b2CdSLVzfBQSH-WieQMMldrA6W61AG73lu-4T7zziROR9i8HYGa8Fyi7fUYc/s1600/Leone+Messi.patapicha.jpg)
Messi alipachika wavuni mabao 60 katika mechi 50 aliyocheza msimu uliopita na hadi sasa amefunga mabao 18 na manane kati ya hayo ndiyo aliyoyafunga katika Ligi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEitg79HW73p7I70v5c5-Z-EIp5ltHvd5U7Laxbas2cGZXJYkMDO6_bFaRM7loIWXfUkXXMDpwW4jQ07f7IzKELOM9qEDdlwcipPGfHkT3cvNYJSYbWfRItpE-rOR1rX20yz3k_4YK9iUWk/s1600/Leonei+Messi.patapicha.jpg)
No comments:
Post a Comment
Ahsante kwa Maoni yako