Monday 23 October 2017

ZIARA YA NAIBU WAZIRI SHONZA

NAIBU WAZIRI WA HABARI JULIANA SHONZA KUSHOTO AKIPATA MAELEKEZO KUTOKA KWA VIONGOZI WA TBC


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Juliana Shonza amewaasa wanahabari kutumia vizuri taaluma yao katika kutoa habari zenye weledi zinazoleta manufaa kwenye jamii na kusisitiza kuwa endapo taaluma hiyo ikitumika vibaya inaweza kusababisha madhara makubwa sana kwa jamii.
Akizungumza wakati wa ziara yake katika makao makuu ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) barabara ya TAZARA jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri Shonza amesisitiza ushirikiano kati ya serikali na wanahabari ili kuipeleka mbele zaidi taaluma ya habari nchini.
Vile vile Naibu Waziri Shonza ameipongeza TBC kwa kuwaamini vijana na kuwapa fursa kubwa ya kufanya kazi na kuendana bega kwa bega na sera ya serikali inayosisitiza kutoa nafasi nyingi kwa vijana katika kulitumikia taifa.
Amesema anashukuru sana kwa ushirikiano aliopewa na TBC na kusisitiza kuwa kwa kushirikiana na Waziri Mwenye dhamana ya wizara hiyo wanashughulikia changamoto zote zinazolikabili shirika hilo.
Ameipongeza TBC kwa kuwa mfano bora miongoni mwa vyombo vingi vya habari nchini na kuviasa vyombo vingine kufuata misingi bora ya taaluma ya habari.
NAIBU WAZIRI AKIWA NDANI YA STUDIO ZA TBC INTERNATIONAL
Hii ni ziara ya kwanza kwa Naibu Waziri Shonza kufika TBC tangu alipoteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli Oktoba saba mwaka huu akichukua nafasi ya Anastazia Wambura.
NAIBU WAZIRI SHONZA ALIPOTEMBELEA STUDIO ZA TBC FM
Habari/picha
Hamisi Hollela na Mahmud Rajab

Wednesday 19 April 2017

NU TRACK

BRAND NEW Track!!!
BADtaito jr Xplastaz & Mstaafrika Presents;
Track: LIVE DIMBANI
Artists: Killa X Gp-Rowdix
Prodution: NOIZMEKAH Arachuga
Genre: Hiphop Asilia
Kupakua wimbo huu mkito BOFYA HAPA

👇🏽👇🏽👇🏽
https://mkito.com/song/16344

#Video Coming Soon.
#Follow Facebook Pg.
@BADtaito jr Xplastaz
@Mstaafrika Arts Music & Culture, Tanzania
Whatsapp: +255758510605
#Support Indigenous Hiphop Tanzania
#BuildersLaneMusic
#EastAfricaCollectiveMovement.
Song Dedicated to all warriors fighting to Expose & Explore real Hiphop worldwide.

Friday 14 April 2017

MBADALA WA BABU WENGER

London, England .Arsenal imeanzisha mazungumzo na kocha wa Juventus, Max Allegri wakati hatima ya Arsene Wenger ikiwa njia panda.
Gazeti la SunSport limebainisha kuwa Gunners imekuwa na mawasiliano na Allegri katika siku saba zilizopita katika kuangalia uwezekano wa kumchukua Mtaliano huyo kushika mikoba ya Wenger.
Hivi karibuni kiongozi moja wa Arsenal alikuwa hafahamu kama Wenger ataendelea kubaki klabu hapo, wakati kocha huyo akiendelea kupata matokeo mabovu na kuongeza shindikizo kutoka kwa mashabiki.
Pia, kuna taarifa kuwa klabu hiyo inahitaji mkurugenzi wa ufundi na winga wa zamani wa klabu hiyo Marc Overmars ametajwa kujaza nafasi hiyo.
Hata hivyo, Wenger anajua kuwa kuna mambo yanayoendelea nyuma yake.
Mwenendo wa kusuasua wa Arsenal kwa sasa umewalazimisha viongozi kumfuatilia Allegri ( 49) mwenye mafanikio makubwa kwa sasa.
Mtaliano huyo ametwaa ubingwa wa Serie A na Kombe la Italia katika misimu yake miwili ya kwanza akiwa na Juventus na sasa pia yuko katika nafasi nzuri ya kutwaa taji msimu huu.
Jumanne iliyopita aliingoza Juventus kuichakaza Barcelona kwa mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.
Jambo zuri zaidi ni kwamba Allegri mwaka jana alimaliza masomo yake ya Kiingereza akiwa ni maandalizi ya kuachana na miamba ya  Serie A na kutimukia Ligi Kuu England.
Kocha huyo pia alikuwa akitakiwa na Chelsea kuziba pengo la Jose Mourinho, lakini kwa bahati mbaya nafasi ikaangukia kwa  Antonio Conte

Friday 7 April 2017

KUTOKA WIZARA YA HABARI UTAMADUNI SANAA NA MICHEZO

Taarifa rasmi kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo juu ya kutoweka kwa wasanii Roma Mkatoliki na Moni Central zone

WASANII ROMA , MONI KUTOKA CENTRAL ZONE NA WATU WENGINE WAWILI WATOWEKA

Wasanii wawili kutoka Tanzania Ibrahim Mussa ajulikanae kama Roma Mkatoliki na Moni pamoja na producer wa Togwe records Bin laden na Emma ambaye ni mfanyakazi wa mama mzazi wa mmiliki wa studio za tongwe records J Murder wametoweka katika mazingira ya kutatanisha wakiwa katika studio hizo za togwe baada ya kuvamiwa na kuchukuliwa na watu wasiojulikana katika gari aina ya noah;J murder ameeleza kushtushwa na tukio hilo na kuongeza kua watu hao walibeba baadhi ya vifaa vya studio na kuondoka navyo.
Baada ya tukio hilo mmiliki wa tongwe rec J Murder alifika kituo cha polisi cha Oysterbay na kuripoti juu ya tukio hilo.

Nae Nancy mke wake roma anaeleza kua simu ya mume wake inaita tu bila kupokelewa na hadi hivi sasa hajui mume wake yupo wapi.
Wasanii kwa umoja wao wameungana kuweza kufatilia swala hilo ambalo hadi hivi sasa hakuna anaejua wasanii hao wako wapi.

Thursday 6 April 2017

NEW TRACK MAUA SAMA

#BrandNewTzVideo Bofya bio ya @mauasama au HAPA https://youtu.be/CO9WYgaeFYg kutazama Official Video ya #MainChick na Pia unaweza kuirequest kwenye vituo vyote vya Tv na radio ..
#supportgoodmusic
#goodmusiclives

Video directed by @khalifan_khalmandro
Produced by @kinglufa
Mastered by #chizanbrain
B RECORDS
Cc @reyjons
@mohchidunga
#MAINCHICK
#InfoPoweredBy #KwanzaPromo #VipajiVMGAfrica @kwanzapromo @teamkaskazi kwanzanetworks.com @vipajivmgafrica @djhazuu djhazuu.com #SapotiNyumbani

NEW TRACK 2017

#BrandNewTzAudio Bofya bio ya @LordEyesmweusi ft @juma_jux au HAPA @mkitodotcom https://mkito.com/song/16272 kupakua wimbo wa #HelaYangu #HelaYanguNtaipataje produced by @kingluffa & @chizanbrain
#InfoPoweredBy #KwanzaPromo @kwanzapromo @teamkaskazi kwanzanetworks.com @djhazuupromo @djhazuu djhazuu.com #SapotiNyumbani