Friday 15 May 2015

HAPPY LOVELY BIRTHDAY DAVID DAVE HOLLELA

Happy birthday to you buddy wishing you happiest life and enjoy your day
God bless you...!

Thursday 14 May 2015

PIC OF THE DAY

Everything Is Possible Under the Sun

HAPPY BIRTHDAY MAMA YETU MAMA SAADA

Imekuwa ni siku njema kwako Allah akujaalie kheri uishi miaka mingi maisha yenye furaha amani na upendo....!
Happy Lovely birthday Twalhiya

Better Muzic

For The Better Muzic Join with NURUMUZIC Production

FAINALI UEFA JUNI 6, NI KATI YA FC BARCELONA VS JUVENTUS


Fainali ya Michuano ya Klabu Bingwa UEFA itafanyika Juni 6, 2015 kwa kuwakutanisha Mabingwa wa Hispania klabu ya Fc Barcelona dhidi ya Wazee wa Turin Juventus katika uwanja wa Olympiastadion, Berlin nchini Ujerumani
Barca waliwatoa Bayern Munich katika hatua ya nusu fainali kwa jumla ya Goli 5-3
Wakati Juventus wamefanikiwa kutinga fainali hizo baada ya kuwaliza Real madrid kwa jumla ya goli 3-2

HALI TETE NCHINI BURUNDI KWA RAIS NKURUNZINZA

Raisi Pierre Nkurunzinza
Tukiangazia hali ya mambo nchini Burundi aliyekua mkuu wa majeshi Jenerali Godefroid Niyombare ametangaza Jumatano hii  kuwa rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza amepinduliwa madarakani.
Hayo yanajiri wakati Rais Pierre Nkurunziza anashiriki mkutano wa kikanda wa marais wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu mgogoro unaoendelea nchini Burundi.
Burundi imekua ikishuhudia maandamano ya raia wakipinga muhula wa tatu wa Pierre Nkurunziza. Kwa muda wa majuma kadhaa mitandao ya kijamii, na vyombo mbali mbali vya habari vimekuwa vikiripoti taarifa hizo kutoka huko Burundi
Mpaka sasa haijajulikana kundi gani lina mamlaka ya uongozi wa nchi, baada ya kundi la wanajeshi linaloongozwa na jenerali Godefroid Niyombare kutangaza kuipindua serikali ya Pierre Nkurunziza.
Hata hivyo Ikulu ya rais huyo imeendelea kutangaza kupitia akaunti yake ya twitter kuwa mapinduzi hayo yamefeli, baada ya jeshi kuingilia kati na kudhibiti hali ya mambo.
Kituo cha habari cha Burundi RTBN kimemhoji rais Pierre Nkurunziza kwa simu mwendo wa saa sita.Vita vimezuka karibu na afisi za kituo hicho cha habari.Jenerali anayeunga mkono jaribio hilo la mapinduzi amekiambia chombo cha habari cha AFP kwamba vitengo vinavyopigana kumpindua vimepata agizo la kukiteka kituo hicho habari cha RTNB kwa kuwa wana uwezo.
Mgogoro wa Burundi umezusha wasi wasi wa kurejea katika ghasia baada ya miaka kumi na miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Zaidi ya watu elfu tatu walikufa katika vita vya kikabila kati ya wahutu na watutsi; vita vilivyomalizwa muongo uliopita.na mgogoro wa sasa nchini humo umehusisha kwa kiasi kikubwa na masuala ya kisiasa. lakini,yaliyojiri Burundi hayana tofauti na kilichojiri katika nchi jirani ya Rwanda ambayo ilikumbwa na mauaji ya kimbari nayo ilikabiliwa na masuala ya ukabila.
Rais Piere Nkurunzinza alizaliwa desemba 18/1963 mjini Bujumbura katika familia ya wahutu

Na baba yake Yustach Ngabisha alikuwa mbunge wa Burundi mwaka 1965 aliuwawa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe mnamo mwaka1972
Jenerali Godefroid Niyombare
Meja Jenerali Niyombare ambae ndie ametangaza mapinduzi hayo nchini Burundi, aliteuliwa kuwa kamanda mkuu wa jeshi la Burundi mwaka 2014  akichukua nafasi ya Adolphe Nshimirimana akiwa anatokea nchini Kenya kama balozi wa Burundi
Lakini alitumuliwa na Nkurunzinza kama mkuu wa usalama February 2015 bila kutolewa sababu za uamuzi huo
Umoja wa mataifa umeonya hivi karibuni kwamba ikiwa ghasia zitasitishwa Burundi itakuwa na Amani na kama itakuwa vinginevyo basi nchi hiyo itarejea katika vita vya wenyewe kwa wenyewe .
watu zaidi ya 20 wameuawa tangu tarehe 25 mwezi uliopita baada ya Nkurunzinza kutangaza kuwania muhula wa tatu madarakani kinyume na katiba ya taifa hilo ambayo inaruhusu mihula miwili tu ya miaka mitano kila mmoja akidai muhula wake wa kwanza alichaguliwa na bunge na wala sio wananchi. Zaidi ya waburundi 50,000 wametorokea nchi jirani kufuatia ghasia za kabla ya uchaguzi wa mwaka huu
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limeitisha kikao cha dharura kujadili hali ya mambo Burundi baada ya jenerali mwandamizi jeshini kutangaza kunyakua madaraka kutoka kwa Rais Pierre Nkurunziza. Kikao hicho cha dharura kimeitishwa na Ufaransa  huku katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon akitoa wito wa utulivu na ustahamilivu nchini Burundi. Wakati huo huo Umoja wa Mataifa unafuatilia kwa karibu kinachoendelea nchini Burundi na kusisitiza kauli ya Katibu Mkuu Ban Ki-moon aliyotoa wakati wa mkutano wa viongozi wa umoja wa Afrika huko Addis Ababa, Ethiopia kuhusu awamu za uongozi.
Hayo ni kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric aliyezungumza mjini New York, wakati wa mkutano na waandishi wa habari waliotaka kufahamu msimamo wa chombo hicho kuhusu hali iliyoripotiwa nchini Burundi.